Monday, January 11, 2010

MAELEKEZO JINSI YA KUANGALIA PESA HALALI

jana nilikuwa na wadau mahali na nikapata shule jinsi ya kuhakiki uhalali wa noti ya sh.(Tz) 10000/=

1)ULE UPANDE WA TEMBO KWA PEMBENI YAANI KUSHOTO KUNA TARAKIMU 10000. TARAKIMU HIZI UNAWEZA KUZIONA TU UKINYANYUA HIYO NOTI KWA JUU

2) UPANDE WA KULIA MWA PICHA YA TEMBO JUU KIDOGO YA TARAKIMU 10000 KUNA MAANDISHI MADOGO SAAAAAAAAANA AMBAYO NIMESHINDWA KUNG'AMUA NI MAANDISHI YA NINI LAKINI HAKIKISHA YAMEONEKANA.

ANGALIZO

nilipochunguza dondoo hizo hapo juu kwenye zile noti feki sikuweza kuziona. Inaonekana kile 'kiwanda uchwara' hakiwezi kuchomeka hizo chachandu.

siku njema.

No comments:

Post a Comment