Friday, January 8, 2010

sauti kutoka kwa kapera

"unatakiwa mwaka 2010 uowe you are grown up"
hii ni kauli ambayo nimeipata humuhumu siku ya leo.Na si leo tu bali kila siku ambayo ndio imenisukuma kuandika hiki ninachokiandika.Naomba kuuliza maswali yafuatayo:
1.Umri gani unafaa kwa mwanaume kuoa na umri wa mwisho mwanaume kuoa ni miaka mingapi?
2.Unaoa ili nini?
3.Unamuoa nani?
4.No regrets/hakuna majuto?
5.Unafuraha?
Ndugu zangu kuoa si kwenda kusafisha nyota ili na wewe uonekane mjini umeoa,mimi naliheshimu sana tukio la ndoa maana ni muunganiko kati ya mwanamke na mwanaume na kuwa kitu kimoja mpaka kifo kitakapowatenganisha kama imani ya dini yangu isemavyo.Mume na mke kufikiri na kutenda kama team moja,kufurahishana,kukasirishana,shida na raha mzipitie pamoja n.k....kuishi na mwenzako miaka nenda rudi ndani ya nyumba moja,chumba kimoja,kitanda kimoja si mchezo kila siku, kuanzisha familia pamoja namengine mengi.Sihitaji kukurupuka kukufurahisha wewe.
Mimi sipo desparate kutaka kuoa am happy na maisha yangu so far,sihitaji mwanamke ndio aje kukamilisha au kuleta furaha katika maisha yangu,am happy with me.
Si kila mwanamke unaekuwa nae kama mpenzi basi lazima umuoe na kuwa mumeo,kuna wakati unakutana na mwanamke mnapendana kabisa lakini kuna vitu ambavyo vinafanya wewe na yeye msiweze kuoana.Kuna ambao si wife material wala mother material.Mwingine hayupo tayari kuolewa muda wake haujafika, mwingine tabia sio zenyewe kabisa.
Am 45 yrs old wala sijihisi kupungukiwa kitu katika maisha yangu...nitaoa muda utakapofika wa kufanya hivyo na mwanamke ambae mimi mtoto p nimeona ananifaa kuwa mke wangu na mama wa watoto wangu.Kwasababu nitapenda kuwa mwanamme mwenye furaha japo najua ndoa ina mapito mengi lakini kama nitakuwa nimeoa mwanamke anaenipenda na mimi kumpenda tutayapita pamoja.
SITAOA ILI KUUDANGANYA ULIMWENGU KUWA NA MIMI NIMEOA...No one is in charge of my happiness except me....my head is my government.

1 comment: