Saturday, January 9, 2010

NOTI FEKI DAR ES SALAAM, TANZANIA


Noti mbili za Tanzanian shillings 10000/=
Hiyo ya kushoto ni feki, ina msitari katikati na inaonyesha kupauka pauka. Nawahatadharisha ndugu na wadau tuwe waangalifu tunapochukua pesa.
Mdogo wangu alichukua 1000,000/= kutoka 'Western Union' na baadaye akakuta 70000/= ni feki.
Ni pale alipoenda kutumia pesa takribani sh. 90000/= ndipo mchuuzi alipomrudishia 40000/= ni kumuelewesha kuwa hizo ni feki. Alipochunguza kale kamilioni kake akagundua 70000/= kati ya hizo ni feki.
Swali kwenu wadau, mbona hizi pesa zilipitishwa kwenye machine? Hiyo machine kazi ya ni nini? mie nilidhani ni kutambua pesa feki.

No comments:

Post a Comment