Friday, January 15, 2010

USHAURI KWA MAKAPERA KUTOKA KWA MDAU GRACE

Hi! Mtukwao!1)

Hakuna umri wa kuoa, ingawa unatakiwa uoe ungali kijana (nguvu) ili kama Mungu atawajalia watoto uwe na wakati mzuri wa kuwajengea msingi wa maisha.

2)Kuoa ni ili kusaidiana kimwili, kimawazo, (kuwa kitu kimoja) na kujenga familia, (kupata watoto) hapo simaanishi kuwa mkioana ni kila mtu anabahatika kupata mtoto au watoto ila ndio tegemeo la wanandoa wengi.

3) Kumuoa nani ni chaguo la mtu mwenyewei.Unamuoa unayempenda au mnayependana ii.mwenye mtavumiliana kwenye shida na raha, *(lako langu, langu lako.)iii. Mtakayeheshimiana (respect matters).

4) Majuto yapo hasa pale utakapogundua kuwa mwenzako mnatofautiana kitabia au hali yoyote ile ambayo inawezafanya mtu akakwazika. i) Kuna mtu unamuoa hujui alikupenda kwa ajili gani pengine kama ni wakati mlikuwa vizuri, akaona umamfaa bila kujua maisha ni kupanda na kushuka leo unacho kesho huna, ninamaana kwamba, kuna wengine hawavumilii shida. Hapo basi ndio hasira zinaanza, kiburi na kutosikilizana. ii) Tabia zako ambazo sio nzuri ulijaribu sana kuzificha na sasa unaziweka azarani yaani hujifichi tena, pia inaleta majuto. Nafikiri nikisema tabia mnanielewa maana hata zingine zimepelekea ndoa nyingi kuvunjika.iii) Kutopata mtoto/watoto inaleta shida pia kama nilivyoekezea kwenye namba mbili mategemeo ya wengi ni kupata familia.iv) Kweli kuna watu wanaoa au kuolewa just a record hajui wajibu wake.

5) Furaha huwepo kutegemeana na nyie wenyewe mnavyoendesha maisha yenu. Hilo nawaachia wanandoa.

Flory nimejaribu kuelezea kwa kifupi au kujibu maswali yako ingawa yako mengi yakuelezea kwa hii topic.Napenda kujua Mother material na mke material yukoje? Je?!! kuna mume material na baba material? lol........

!Grace

2 2gether are always better than he wu is alone

No comments:

Post a Comment