Tuesday, September 29, 2009

usafiri kijijini

Kwa usafiri huu, kelele za global pollution hazitakuwepo. Kwanini Dar Es Salaam usafiri wa baiskeri siyo maarufu? there's serious dent on our city plan!!!! pale uingereza mwendesha baiskeri anapewa heshima yake kama mwenye gari. hapa Tanzania? baiskeri ni ya vijijini.
Lakini kama Msomi Ali Mazrui alivyowahi kusema, 'The only thing we as africans need to change is our own changebility'; muda wote tunabadilisha mazingira yetu yaendane na mazingira ya wanaotutawala.
Leo Dar inangara kwa prado, Vx, hammer, na magari kibao ya Fwd kutoka japan, wakati hao hao wageni waliotupa baiskeli ndio wanaotupa magari. Bado barabara zetu hazikutengenezwa kwa ajili ya waendesha baiskeri. Barabara hasa za Dar ni nyembamba kuruhusu magari na baiskeri kupita kwa wakati mmoja. Na hata pale mjasiri anapoamua kuendesha baiskeri, ana hatarisha maisha yake kwa vile madereva wetu wanatumia njia hizo hizo zinazotegemewa kutumia waendesha baiskeri.

No comments:

Post a Comment